Monday 30 November 2015

#YALIYOJIRI>>Rais John Magufuli Akutana na Mabolozi Wa China na Korea Kusini,Ahakikishiwa Ujenzi wa Daraja la Salender Dar-es-salaam.Fahamu zaidi hapa.

Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Balozi wa China hapa nchini Dkt. Lu Youqing, Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 30, 2015.
 Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiwa katika mazungumzo na Balozi wa China hapa nchini Dkt. Lu Youqing, Ikulu jijini Dar es salaam leo Novemba 30, 2015.
Vichwa vya habari za siasa Tanzania bado vinaendelea kubeba stori kila mara kuhusu Rais John Maguful. inawezekana ni kawaida kabisa kila siku kukutana na habari zaidi ya tatu au nne kuhusu Rais John Maguful tangu siku ya kwanza alipoapishwa na kuanza kazi ya Urais wa Tanzania.
 
Ninayo nyingine kutoka Ikulu sasahivi, hii inahusu Rais John Maguful kumuaga Balozi wa Korea Kusini, Chung IL ambapo Balozi huyo amemhakikishia Rais Magufuli kwamba daraja hilo litajengwa kwa ufadhili wa Serikali yake.
 

0 comments:

Post a Comment