Thursday 5 November 2015

#YALIYOJIRI>>>Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe awasili Tanzania kuudhulia sherehe za kuapishwa John Pombe Magufuli.Fahamu zaidi hapa.

 Waziri Membe akimpokea Rais Mugabe (mwenye Ua Mkononi) mara tu baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julias Nyerere jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Bernard Membe (katikati chini) akimsubiria Rais wa Zimbabwe Mhe. Robert Mugabe (katikati juu kwenye ngazi) alipokuwa akiteremka kwenye Ndege, Rais Mugabe amewasili nchini kwaajili ya kuhudhuria Sherehe za uapisho wa Rais Mteule Mhe.Dkt. John Pombe Magufuli zitakazofanyika hapo kesho katika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
 Mhe. Netumbo Nandi - Ndaitwah (wa pili kutoka kulia) akifurahia kikundi cha ngoma kilichopo mbele yao.
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe (kushoto) akimlaki Naibu Waziri Mkuu wa Namibia Mhe. Netumbo Nandi - Ndaitwah mara baada ya kuwasili nchini kwa ajili ya kushuhudia Uapisho wa Rais Mteule Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.
  Afisa Mambo ya Nje Bi. Liliani Kimaro akisalimiana na Rais wa Zimbabwe Mhe. Robert Mugabe.
 Rais wa Zimbabwe Mhe. Robert Mugabe akikagua Gwaride la Heshima.
 Rais wa Zimbabwe Mhe. Robert Mugabe akiangalia kikundi cha wapiga Tarumbeta huku Waziri Membe akitoa ufafanuzi wa nyimbi iliyokuwa inachezwa. 
Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini pia anayeiwakilisha Tanzania nchini Botswana Mhe. Radhia Msuya (kushoto) akisalimiana na Makamu wa Rais wa Botswana Mhe. Olale Eric Mothibi alipo wasili nchini kwaajili ya kushiriki Sherehe za Uapisho wa Rais Mteule Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.

0 comments:

Post a Comment