Thursday 21 July 2016

#MICHEZO>>>LIVERPOOL YASAJILI MBADALA WA TOURE.Fahamu zaidi hapa.

Liverpool wamefanikiwa kumnasa beki Ragnar Klavan kutoka klabu ya Augsburg ya Ujerumani kwa mkataba wa miaka mitatu.

Klavan (30) ambaye amesajiliwa na ada ya paundi milioni 4.2 ataungana na wenzake Jumanne ijayo nchini Marekani ambapo wameweka kambi kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya wa ligi.

Beki huyo mwenye uzoefu mkubwa amesajiliwa kwa jili ya kusaidiana na Mamadou Sakho na Joe Gomez ambao kwa sasa wanasumbuliwa na majeraha

Atakuwa akivaa jezi namba 17 ambayo awali ilikuwa ikivaliwa na Sakho

Nahodha huyo wa Estonia anakuwa mchezaji wa tano kusajiliwa na Liverpool msimu huu huku akiwa ni mchezaji wa tatu kusajiliwa kutoka Bundesliga chini ya utawala wa Klopp.

0 comments:

Post a Comment