Home »
Michezo
» #MICHEZO>>>>USAJIRI UINGEREZA KUHUSU POGBA KUTUA OLD TRAFFORD.Fahamu zaidi hapa.
Paul Pogba anatua Manchester United
Siku nyingine tena Paul Pogba yuko kwenye kurasa za mbele za magazeti ya Ulaya.
Gazeti la La Gazzetta dello Sport la nchini Italy limeandika habari
ambayo huenda ikawakosha mashabiki wa Manchester United kuhusu kiungo
huyo wa kimataifa wa Ufaransa mwenye miaka 23 kurejea kwenye himaya ya
Old Trafford
Kichwa cha habari cha gazeti hilo kinaashiria kwamba Juventus
wanamuuza Pogba kwenda United huku wakifanya mipango ya kumnasa
mshambuliaji wa Napoli Gonzalo Higuain kutua Turin.
Habari mpya kuhusu dili la Pogba kutua United
Ukisoma habari hiyo kwa undani inasisitiza kwamba, wakala wa Pogba
Mino Raiola ameshasafiri kwenda England kusikiliza ofa ya Man United juu
ya mteja wake.
Ofa kutoka Old Trafford ni euro milioni 100 huku kukitarajiwa kuwa na nyongeza ya euro 24 nyingine.
Ongezeko hilo la euro milioni 24 halijawekwa wazi ni kwa ajili ya
nini, lakini inawezekana wanaweza kuweka kipengele cha kuongezewa
mkwanja iwapo Pogba ataisaidia United kushinda taji la Champions League
au kama atafanikiwa kutwaa Ballon d’Or.
Pogba anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka mitano kuitumikia United
ambapo atavuna kitita cha euro milioni 12 kwa msimu kutokana na
mshahara.
Related Posts:
#MICHEZO>>>CHEKI ZAZA ALIVYOKAMILISHA NA KUTUA WEST HAM, SUBIRI MAMBO YAKE.FAHAMU ZAIDI HAPA.
West Ham wamekamilisha usajili wa mshambuliaji Simone Zaza kutoka Juventus ya Italia.
West Ham inayoshiriki Ligi Kuu England, imetoa pauni milioni 4.3 ingawa dili lenye litahusisha jumla ya pauni million 17.
… Read More
#MICHEZO>>>>RASHFORD AFUNGA BAO DAKIKA YA MWISHO, MAN UNITED YAIBUKA NA USHINDI WA BAO 1-0 DHIDI YA HULL CITY.FAHAMU ZAIDI HAPA.
Hull City (4-3-3): Jakupovic 7;
Elmohamady 6, Davies 8, Livermore 6.5, Robertson 6; Huddlestone 6.5,
Meyler 7, Clucas 6; Snodgrass 6.5 (Maloney 48 6), Hernandez 6.5 (Maguire
83), Diomande 6.5
Substitutes: Kuciak … Read More
#MICHEZO>>> Jose Mourinho Ampiga Mkwara Rashford.Fahamu zaidi hapa.
MWACHENI Jose Mourinho na kiburi chake aisee. Ungeweza kudhani angetoa
maneno ya kufariji kwa kinda Marcus Rashford baada ya juzi kuibuka na
ushujaa wa dakika za mwisho katika pambano gumu dhidi ya Hull City
ugenini. Mou… Read More
#MICHEZO>>>>ALICHO ONGEA WYNE ROONEY BAADA YA KUSIKIA NDUGU YAKE KAPANDA MLIMA KILIMANJARO.FAHAMU ZAIDI HAPA.
August 18 2016 ilikuwa ni siku ya kihistoria kwa Anthony McLoughlin ambaye ni shemeji wa mshambuliaji wa kimataifa wa England anayeichezea Man United Wayne Rooney, Anthony August 18 alifanikiwa kupanda mlima Kilimanjar… Read More
#MICHEZO>>>>MKWASA AMPUMZISHA DIDA TAIFA STARS, YULE KIPA MTAMU WA JKT APATA ULAJI.FAHAMU ZAIDI HAPA.
Kocha
Mkuu wa timu ya Mpira wa Miguu Tanzania ‘Taifa Stars’, Charles Boniface
Mkwasa, amefanya mabadiliko kwenye kikosi kinachotarajiwa kusafiri
Jumatano Agosti 31, 2016 kwenda Nigeria kwa ajili ya mchezo wa mwisho wa
… Read More
0 comments:
Post a Comment