Home »
Habari Moto
» #YALIYOJIRI>>>Hali Ngumu ya Maisha, Afisa wa Polisi Ajiua Kwa Kujipiga Risasi Jomo Kenyatta (JKIA).Fahamu zaidi hapa.
Afisa wa polisi Caudencia Wausi alimejiua kwa kujipiga risasi kichwani
katika uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta (JKIA) muda mfupi baada ya
kuchapisha ujumbe wa kuashiria kuwa na mahangaiko maishani.
Koplo Caudencia Wausi alitumia bastola yake aina ya Jericho kujifyatulia
risasi kichwani ndani ya choo dakika 13 tu baada ya kuchapisha ujumbe
katika mtandao wake wa Facebook.
"Maisha ni magumu unapoishi katika ulimwengu ambapo kila mtu anapanga
kukufanyia maovu.. na utafanya nini wakati ambapo huwezi kuvumilia au
hauna uwezo wa nguvu za kuwatia nguvu wapendwa wachache katika maisha
yako.!? hauna lingine la kufanya ila... kwa hivi nisadie Mungu
"aliandika kwenye Facebook.
Kwa mujibu wa mkubwa wake, Bi Wausi alikuwa amerudi kazini kutoka mapumzikoni kabla ya kujiua baada ya kujifungia chooni, JKIA.
Inadaiwa alijifungua mkanda wake wa polisi na kuuacha katika chumba cha
Control Room pamoja na fimbo yake kabla ya kujifungia chooni.
"Tulisikia tu mlio wa risasi na baadaye tukampata juu ya choo huku
bastola yake ikiwa mkononi, alikuwa tayari ameaga dunia "alisema kamanda
wa polisi katika uwanja wa ndege Rono Bunei.
Bwana Bunei alisema kisa hiki kimeshtua wenzake kwasababu afisa huyo hakuwa na dalili za kusongwa na mawazo.
" Alikuwa anapiga gumzo na wenzake asubuhi na nilimuona mwenye furaha,
hakuonyesha dalili zozote za kuwa na mahangaiko "alisema Bw Bunei na
kuongeza kuwa uchunguzi umeanza kubaini kilichosababisha afisa huyo
kujiua.
Related Posts:
#YALIYOJIRI>>>Watu Wenye Ulemavu wa ngozi kuwafukuzisha Kazi Wakuu wa Wilaya , Mwanza Seebait.com 2016.Fahamu zaidi hapa.
Mkuu
wa mkoa wa Mwanza John Mongella, amewaapisha wakuu wapya wa Wilaya za
Mkoa wa Mwanza na kuwapa vitendea kazi ikiwapo katiba ya Jamhuri ya
muungano wa Tanzania na Ilani ya Chama Tawala Chama Cha Mapinduzi (CCM)
ya … Read More
#YALIYOJIRI>>>>Mahakama Yawataka Wabunge Halima Mdee na Mwita Waitara kuheshimu taratibu za kisheria.Fahamu zaidi hapa.
Mahakama
ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, imetoa onyo kwa Wabunge Halima
Mdee (Kawe) na Mwita Waitara (Ukonga) kwa kushindwa kufika mahakamani
kusikiliza kesi inayowakabili dhidi ya kumjeruhi Kat… Read More
#YALIYOJIRI>>>Agizo La Kuzuia Uvutaji Wa Sigara Na Matumizi Ya Bidhaa Za Tumbaku Katika Maeneo Ya Umma.Fahamu zaidi hapa.
Wizara
ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inampongeza
Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kwa kupiga
marufuku matumizi ya Shisha na uvutaji wa Sigara hadharani kama afua ya
kupunguz… Read More
#YALIYOJIRI>>>Shahidi akwamisha Kesi ya IPTL dhidi ya Zitto Kabwe.Fahamu zaidi hapa.
Kampuni
ya kufua umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) ilifungua
kesi ya madai ya fidia ya Sh. bilioni 500 Mahakama kuu, kanda ya Dar es
Salaam dhidi ya Zitto Kabwe.
IPTL pamoja na wadai we… Read More
#YALIYOJIRI>>>>Maiti Yazuiliwa hospitali ya Muhimbili ikidaiwa fedha.Fahamu zaidi hapa.
Hospitali
ya Taifa Muhimbili imegoma kuruhusu mwili wa marehemu Bi Hilda Lukas
miaka 30 aliyefariki dunia June 26 katika hospitali hiyo, akisumbuliwa
na ugonjwa wa utumbo kutoboka huku ikidai lazima fedha yote wanayomd… Read More
0 comments:
Post a Comment