Home »
Habari Moto
» #YALIYOJIRI>>>>JAJI WARIOBA AAMUA KUMJIBU HIVI MZEE KINGUNGE.FAHAMU ZAIDI HAPA.
Siku moja baada ya Mwanasiasa mkongwe, Mzee Kingunge Ngombale Mwiru
kuwaomba viongozi wastaafu kumshauri Rais John Magufuli kuikutanisha
Serikali na Chadema ili kuvunja UKUTA kwa amani, Jaji Joseph Warioba
amejibu.
Jaji Warioba amesema kuwa suala hilo lisichukuliwe kama tatizo la Rais John Magufuli pekee bali ni tatizo la watu wote nchini.
“Ni wajibu wa Watanzania wote kuhakikisha wanalinda hali ya amani
nchini badala ya kuliona hilo… kusema jambo hili halimhusu Rais John
Magufuli pekee, linamhusu mtu mwingine yeyote. Tumsaidie msajili katika
hili, hili sio tatizo la mtu mmoja bali ni la nchi nzima, tusimuachie
Rais wetu,” Jaji Warioba amekaririwa.
Amesema kuwa badala ya kumjibu Mzee Kingunge, ni vyema kumpa nafasi
Msajili wa vyama vya siasa nchini, Jaji Francis Mutungi kuwakutanisha
viongozi wa vyama vya siasa ili kujadili kwa lengo la kutafuta muafaka.
Aidha, Jaji Warioba alisema kuwa wao kama wazee wamekuwa wakimshauri
Rais kwa mambo mengi, lakini ushauri huo hawautoi kupitia vyombo vya
habari.
“Kweli tuko kimya lakini ukimya huo usitafsiriwe vibaya kuwa
hatumshauri Rais Magufuli, sisi kama viongozi wastaafu tunamshhauri rais
lakini sio katika vyombo vya habari,” alisema
Related Posts:
#YALIYOJIRI>>>BASATA yaufungia wimbo wa Nay wa Mitego ‘Shika Adabu Yako’.Fahamu zaidi hapa.
Baraza
la Sanaa la Taifa (BASATA) limeufungia rasmi wimbo wa ‘Shika Adabu
Yako’ ulioimbwa na Msanii Nay wa Mitego kutokana na ukiukwaji mkubwa wa
maadili, kashfa, uchochezi, kudhalilisha watu na kuhatarisha amani na
ut… Read More
#YALIYOJIRI>>>CCM Yalaani Vikali Kitendo Cha Kuwekwa Alama ya X Kwenye Nyumba Za Wafuasi Wake.Fahamu zaidi hapa.
CHAMA CHA MAPINDUZI kimelaani vikali kitendo cha kuwekwa alama ya X kwenye nyumba za wafuasi wake Kisiwani Pemba.Pia CCM imesikitishwa na kulaani vikali kitendo cha kuchoma moto tawi la CCM la Kengeja.Katibu
wa Kamati Maa… Read More
#YALIYOJIRI>>>ZEC Yagoma Kuondoa Picha ya Maalim Seif Kwenye Karatasi za Kura CUF Yasema Ipo Tayari Kwa Mazungumzo ila Sio Kurudia Uchaguzi.Fahamu zaidi hapa.
Zikiwa zimebaki siku chache kabla ya kurudiwa kwa uchaguzi Zanzibar,
Makamu wa Kwanza wa Rais Maalim Seif Sharrif Hamad amehoji sababu za
chama tawala, CCM kuhofia CUF kuongoza visiwa hivyo.
Maalim
Seif, amba… Read More
#YALIYOJIRI>>>TAKUKURU Yawafikisha Mahakamani Vigogo 11 wa Kampuni ya Reli (TRL).Fahamu zaidi hapa.
Hatimaye
vigogo 11 wa Kampuni ya Reli (TRL) waliosimamishwa kazi hapo awali
wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
wakishtakiwa na makosa tisa yakiwemo matumizi mabaya ya madaraka
yaliyopelekea … Read More
#YALIYOJIRI>>>Mwanamke Aliyemkaba Jambazi Na Kumpora Bunduki Aina Ya SMG Azawadiwa Laki 5 Na Jeshi La Polisi.Fahamu zaidi hapa.
Mwanamke aliyepambana na jambazi na kufanikiwa kumnyang’anya bunduki
aina ya SMG, Sophia Manguye (46), amepewa zawadi ya Sh 500,000 na
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu Tarime/Rorya, Gemini Mushy.
Mwanamke
huyo ambaye a… Read More
0 comments:
Post a Comment