Home »
Habari Moto
» #YALIYOJIRI>>>>>Bosi wa TPDC Asimamishwa Kazi.Fahamu zaidi hapa.
BODI ya Wakurugenzi ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC)
imemsimamisha kazi Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo, Dk James
Mataragio.
Taarifa za uhakika kutoka ndani ya shirika hilo na wadau mbalimbali wa
masuala ya mafuta na gesi, zimeeleza kuwa kusimamishwa kazi kunatokana
na ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu (CAG) ya mwaka jana iliyoeleza
kuwa, TPDC ilikiuka taratibu za manunuzi ya umma kwa kuipa upendeleo
kampuni ya Marekani kutafiti mafuta na gesi katika maeneo ya kaskazini
na magharibi mwa Ziwa Tanganyika, Songosongo, Mandawa na Eyasi.
“Shirika kwa sasa si salama, kwani mkurugenzi amepewa barua kutoka kwa
mwenyekiti wa bodi kusimamishwa kazi kuanzia jana (Jumatano) kutokana na
ripoti ya ukaguzi,” alisema mmoja wa watoa taarifa.
Hata hivyo, mpaka jana jioni hakukuwa na taarifa rasmi kuhusu kusimamishwa kazi kwa mkurugenzi huyo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Justin Ntalikwa
alipoulizwa kuhusu hatua hiyo, alisema anafahamu suala la kusimamishwa
kazi kwa Dk Mataragio, lakini akaongeza kuwa, maelezo zaidi kuhusu
maamuzi hayo anayo Mwenyekiti wa Bodi ya shirika hilo, Profesa Sufian
Bukurura.
Hata hivyo, Mwenyekiti huyo alipotafutwa kwa simu kutoa taarifa rasmi za
kusimamishwa kazi kwa mkurugenzi huyo, hakupatikana kwani mara zote
simu yake ilisema inatumika.
Related Posts:
#YALIYOJIRI>>>>Lowassa, Mbowe Watakiwa Kuripoti Polisi Keshoi Septemba 1.Fahamu zaidi hapa.
Mwenyekiti
wa Chadema, Freeman Mbowe, Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama hicho, Edward
Lowassa na viongozi wengine waandamizi wameitwa na Jeshi la Polisi Kanda
Maalumu ya Dar es Salaam kwenda kuripoti kesho Septemba Mosi.
… Read More
Weka Picha za Utupu Mtandaoni Uende Miaka 20 jela – TCRA.Fahamu zaidi hapa.
Unataka kwenda jela? Ni rahisi, weka picha za ngono mtandaoni, na utakuwa mkazi wa huko kwa kipindi cha miaka 20.
Kwa mara nyingine tena, mamlaka ya mawasiliano Tanzania, TCRA
imewakumbusha watanzania kutozichezea sharubu… Read More
#YALIYOJIRI>>>>Ndege za Kivita Kutawala Anga la Dar Septemba 1.Fahamu zaidi hapa.
Septemba
mosi mwaka huu inataraji kuingia katika histori ya Tanzania kutokana na
matukio ambayo yanataraji kufanyika siku hiyo, matukio hayo ni pamoja
na sherehe za miaka 52 ya Jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ),
maa… Read More
#YALIYOJIRI>>>Jukwaa la wahariri lalaani Serikali kufungia redio.Fahamu zaidi hapa.
… Read More
#YALIYOJIRI>>>>Lowassa Atoa Waraka Kuhusu Kukamatwa Kwake.Fahamu zaidi hapa.
WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowassa ametoa waraka akisema kitendo cha
askari wa Jeshi la Polisi kuwakamata wakati wakiwa kwenye kikao cha
ndani cha Chadema jana kimemuimarisha na kumpa nguvu zaidi ya kudai
demokr… Read More
0 comments:
Post a Comment