Home »
Habari Moto
» #YALIYOJIRI>>>>Jeshi la Polisi lasema mauaji ya Askari wanne Mbagala yanahusishwa na Operesheni UKUTA.Fahamu zaidi hapa.
Kamishna Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi Nsato Marijan
amesema kuwa mauaji yaliyotokea jana usiku katika benki ya CRDB Mbande
Mbagala yanahusishwa na Operesheni UKUTA iliyotangazwa na viongozi wa
vyama vya upinzani.
Marijan ameyasema hayo leo akizungumza na waaandishi kuhusu mauaji ya
Askari wanne waliouawa jana usiku ambapo amesema kuwa viongozi wa vyama
vya siasa wamekuwa wakihamasisha wafuasi wao kuwashambulia Maafisa wa
Jeshi la Polisi hivyo kutokea kwa tukio hilo huenda kuna uhusiano na
maneno hayo yanayotolewa.
Kufuatia hatua hiyo, Jeshi la Polisi nchini limepiga marufuku
mikutano au vikao vyote vya ndani ya vyama vya siasa kutokana na matukio
ya kihalifu kutokea.
Katika hatua nyingine Jeshi la Polisi limekiri kuwa mazoezi ambayo
yamekua yakifanywa na Askari wake katika maeneo tofauti tofauti ya nchi
ni kwa ajili ya kukabiliana na waandamanaji Septemba Mosi na matukio
mengine ya kihalifu.
Katika tukio la mauaji, Askari wanne waliuawa jana usiku na majambazi
na kisha kutoweka na silaha na kwenda kuvamia kituo cha polisi na
kuondoka na silaha pamoja na sare za polisi. Maaskari hao waliouawa
walikuwa wakibadilishana lindo na wenzao waiokuwa wakati wa mchana.
Related Posts:
#Breaking News>>>>Rais Magufuli Amteua Anne Kilango Malecela Kuwa Mbunge..!!!!..Fahamuj zaidi hapa.
Rais John Magufuli amemteua Anne Kilango Malecela kuwa mbunge, huku
akiwa mkuu wa mkoa pekee kwenye utawala wa awamu ya tano aliyedumu na
wadhifa huo kwa muda mfupi wa siku 29.
Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Rais… Read More
Mbowe kitanzini tena,apewa siku 14 kulipa deni linalomkabili.Fahamu zaidi hapa.
Miezi
takribani mitano iliyopita tangu aondolewe Billcanas, siku moja tangu
Serikali imzuie asiendelee na shughuli za kilimo katika shamba lake,
Mwenyekiti huyo wa Chadema amepewa siku 14 awe amelipa kodi
inayokadiriwa… Read More
Nyumba ya Mbunge wa CCM Yabambwa Kwa Wizi wa Umeme..!!!..Fahamu zaidi hapa.
SHIRIKA la Umeme Tanzania
(Tanesco) limebaini wizi wa umeme katika nyumba ya aliyekuwa Mbunge wa
Mtwara Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Hasnain Murji.
Mhandisi
wa Tanesco Mkoa wa Mtwara, Fabiani Ruhumbika, ali… Read More
Rais wa Uturuki awasili leo na kupokelewa na waziri mkuu.Fahamu zaidi hapa.
RAIS wa Uturuki Mheshimiwa Recep Erdogan amewasili nchini leo
jioni (Jumapili, Januari 22, 2017) kwa ziara ya kikazi ya siku mbili na
kupokelewa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere na
kupokelewa na W… Read More
Rais wa Uturuki Aleta Neema Tanzania...!!!..Fahamu zaidi hapa.
Wakati Rais wa Uturuki, Recep Erdogan
akitua nchini leo, uhusiano kati ya nchi yake na Tanzania umesaidia
kukua kwa biashara kutoka Dola66 milioni za Marekani (zaidi ya Sh 135
bilioni) hadi Dola180 milioni (zaidi ya Sh3… Read More
0 comments:
Post a Comment