Thursday 17 December 2015

#YALIYOJIRI>>Vigogo Watatu wa TRA Akiwemo Tiagi Masamaki Waachiwa Kwa Dhamana Baada ya Kutimiza Masharti.Fahamu zaidi hapa.

Hatimaye vigogo watatu wa mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) akiwemo kamishna wa forodha na ushuru wa mamlaka hiyo, Tiagi Masamaki wameachiwa  kwa dhamana na mahakama ya hakimu mkazi Kisutu, baada ya kutimiza masharti ya dhamana yaliyotolewa mahakama kuu ya Tanzania kanda ya Dar es Salaam.
 
Washtakiwa hao wamedhaminiwa kwa sh. Bilioni 6.6, na hati za mali zisizohamishika zilizowasilishwa katika mahakama ya Kisutu ambapo dhamana ya vigogo hao imetolewa na hakimu mkuu mfawidhi wa mahakama ya Kisutu, baada ya washtakiwa kutimiza masharti ya dhamana yaliyotolewa na jaji wa mahakama kuu Winfrida Koroso.

Jaji Koroso alisema ili washtakiwa wawe nje kwa dhamana kila mwombaji alitakiwa aweke mahakamani sh. Bilioni 2.1 au hati za mali isiyohamishika zenye thamani hiyo na wadhamini wawili watakaosaini dhamana ya sh. Milioni 20.

Baada ya hati hizo kuwasilishwa mahakamani hapo, hakimu alikubaliana na hati hizo na kuwapatia washtakiwa dhamana, lakini wakili wa serikali Christopher Msigwa aliomba mahakama hati hizo zikafanyiwe  uhakiki kwa sababu zingine anamashaka nazo.

Aidha wakili Msigwa amedai kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na itatajwa Desemba 30 mwaka huu.

Washtakiwa ambao hawajaomba dhamana na wamerudishwa rumande na mahakama kuu ni msimamizi mkuu wa ICD-Azam, Eliachi Mrema, mchambuzi mwandamizi wa masuala ya biashara TRA, Khamis Omary, Haroun Mpande wa kitengo cha mawasiliano ya kompyuta ICT - TRA, meneja uendeshaji usalama na ulinzi wa Azam ICD, Raymond Louis na meneja Azam ICD, Ashraf Khan.

Desemba 3, mwaka huu, Masamaki na wenzake walipandishwa kizimbani katika mahakama ya Kisutu, wakikabiliwa na mashitaka ya kula njama ya kudanganya na kuisababishia serikali hasara ya sh. Bilioni 12.7 kutokana na makontena 329 kukwepa kodi.

0 comments:

Post a Comment