Thursday 29 September 2016

Je, Wivu ni Dalili ya Mapenzi ya Dhati au Roho Mbaya?..Fahamu zaidi hapa.

Leo nimekutana na huu mjadala mahali ulionifanya nilete hilo swali hapo juu.
Ni hivii, nimekutana na mtu siku za karibuni na kuanzisha urafiki wa kawaida tu. Sasa katika mazungumzo likaja swala la mapenzi na wivu. Mwenzangu anaamini kuwa na wivu sio mapenzi kwa kuwa, wivu ni dalili ya kumnyima mwenzio kupata kile roho inapenda. Kwamba, kwake yeye hata kama ikitokea akaoa, hatomnyima mke wake kutembea na mwanaume mwingine yeyote atayependa. Tena ikibidi atume na video kabisaa ili impe stimu wakati manzi ake analiwa.

Wakuu, je ni kweli wivu ni dalili ya uchoyo? Na kwamba kama unampenda mtu kwa dhati huwezi kuwa mchoyo kwake. Kule uzunguni mume/mke huwa wanapeana nafasi ikitokea mmoja wapo kamtamani mtu mwingine wanakubaliana kuonja. Tuwaeleweje hawa watu? Maana ni binadamu wenzetu.

Nawasilisha hoja kwa majadiliano.

Karibuni

0 comments:

Post a Comment