Thursday 29 September 2016

#YALIYOJIRI>>>>SERIKALI YATAKIWA KUPUNGUZA KODI VIFAA VYA INTERNET.FAHAMU ZAIDI HAPA.

SERIKALI imeshauriwa kupunguza ushuru wa vifaa vinavyotumia intaneti ili kuongeza kasi ya maendeleo ya shughuli za kiuchumi na kijamii zinazotegemea huduma hiyo.

Wito huo umetolewa Dar es Salaam na Mkurugenzi Mkazi wa Kampuni inayotoa huduma za mitandao ya Ericsson, Frode Dyrdal, wakati wa uzinduzi wa mitambo ya gharama nafuu ya kusambaza intaneti.

Alisema huduma ya intaneti inasaidia kuendeleza sekta za elimu, afya, fedha na burudani, hivyo ni kiungo muhimu katika kuinua uchumi wa nchi.

“Wakati sisi tunajitahidi kuhakikisha upatikanaji wa intaneti kwa gharama nafuu, ni vyema serikali ikaangalia namna ya kuwafanya watu wengi wawe na vifaa vinavyotumia intaneti na njia mojawapo ni kupunguza ushuru wa bidhaa za aina hiyo”, alisema.

Alisema utafiti unaonesha kwamba ni watu wanne kati ya 10 ndio wanaoweza kupata intaneti barani Afrika.

Akizungumzia kuhusu mitambo yao, alisema imelenga kutatua changamoto za upatikanaji mdogo, maendeleo endelevu na gharama kubwa za huduma ya intaneti nchini.

0 comments:

Post a Comment