Friday 23 September 2016

#YALIYOJIRI>>>>Lowassa awajulia hali wahanga wa tetemeko Bukoba hii leo.Fahamu zaidi hapa.

Edward Lowassa akiwapa pole wahanga wa tetemeko akiwa ameenda kuwapa mkono wa pole ya tetemeko la ardhi ambalo limewakumba.

Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Edward Lowassa, leo amewasili Bukoba mkoani Kagera kuwatembelea na kuwajulia hali waathirika wa tetemeko la ardhi.


Tetemeko la ardhi lililotokea Bukoba mkoani Kagera Septemba 10 lilisababisha vifo vya watu 19 huku wengine zaidi ya 250 wakiachwa na maejeraha mbalimbali.

Alipofikika katika uwanja wa ndege wa Bukoba, Edward Lowassa aliyeambatana na  Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema , Sheikh Katimba, Khamis Mgeja na Mbunge wa Bukoba Mjini, Wilfred Lwakatare waliongozana hadi eneo la Hamugembe na Kashai kujionea madhara ya tetemeko la ardhi.

Akizungumza kwa nyakati tofauti na wananchi wa maeneo hayo, Lowassa aliwapa pole sana kwa yote yaliowafika na kusisitiza kwamba anaamini serikali itachukua jukumu la kuwasaidia.

Aidha, amesema kuwa msaada wake yeye atampatia Mkuu wa Mkoa, Meja Jenerali Mstaafu, Salum Kijuu ili uweze kuwasaidia wananchi wa Kagera.
Edward Lowassa akiwa anawasili Bukoba hii leo.
Lowassa akiwa kwenye ndege kuelekea Bukoba sambamba na Shekh Katimba hii leo.

<<<<DOWNLOAD APPLICTION KWENYE SIMU YAKO HAPA>>>

0 comments:

Post a Comment