Home »
Habari Moto
» Diamond Amaliza ziara ya Ulaya, Adai Reality TV Show yake itaweka Wazi Mambo Mazito.Fahamu zaidi hapa.

Diamond Platnumz amemaliza ziara yake ya Ulaya aliyoipa jina, From
Tandale to The World Tour iliyompeleka kwenye nchi takriban nane.
Show yake ya mwisho ilifanyika Jumamosi hii jijini Copenhagen, Denmark ambayo video zake inaonesha ilikuwa na mafanikio makubwa.
Mchumba wake Zari aliyemsindikiza kwenye nchi zote alizopita, ameshukuru
kwa kuandika: Allow me to thank everyone that helped us while out there
in Europe. For showing us around and hosting us. Mostly thank you for
allowing my hubby entertain you. Stay blessed.
Tayari Zari amerejea Afrika Kusini kuungana na familia yake.
Katika hatua nyingine Diamond amedai kuwa reality TV show yake ijayo itaweka wazi mambo mengi mazito.
“Can you try to guess the name of our Reality Show?) (Muda si Mwingi
Kipindi cha Maisha yangu ya kila siku, Familia na Team yangu nzima
itaanza kuwa kwa Tv yako pendwa, ” ameandika Instagram.
“Nakuahidi sio tu eti Kireality show … ni Reality show Bora ambayo
naamini utaipenda kunzia kwenye Quality, Mikasa na matukio yote
nnayopitia mimi, Familia na Team yangu kila siku….Mengi yanaonekana,
Unayoyasikia, Unayasoma ila kwenye Hiki kipindi ndio itakuwa Thibitisho
la kila uvumi uusikiao….Sjui Kipini puani, Mara jicho, Mara sjui
@officialshetta , Mara DNA, Mara @romyjons kutoinekana tena kwenye Tour
Ghafla….Niamini mimi yote utaona na kuyapata kwa uwazi kabisa, Kaa na
Mimi…….! We unavyohisi reality Show yetu itakuwa inaitwaje…..?”
ameongeza
Related Posts:
#YALIYOJIRI>>>>Serikali Yaiamuru Bodi ya Mikopo Istishe Makato na Imlipe Pesa Zake Mstaafu Aliyekuwa Akikatwa Kimakosa.Fahamu zaidi hapa.
Serikali
imeiagiza Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu kusitisha mara
moja makato ya fedha yaliyokuwa yakifanywa kwenye malipo ya pensheni ya
mstaafu Ernest Lameck, katika Chuo cha Ualimu cha Tukuyu kilich… Read More
#YALIYOJIRI>>>>Makontena 100 Yapitishwa Kinyemela Bandarini Bila Kukaguliwa .....Waziri Mwijage Atoa Siku 4 Wahusiku Wajisalimishe.Fahamu zaidi hapa.
WAZIRI
wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage ametoa siku nne kwa
wafanyabiashara waliopitisha makontena 100 bandarini bila kukaguliwa na
Shirika la Viwango Tanzania (TBS), wakatoe taarifa katika shirika.
… Read More
#YALIYOJIRI>>>Mbowe kuiburuza Serikali mahakamani.Fahamu zaidi hapa.
Mwenyekiti
wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amesema
ataiburuza Serikaliya Awamu ya Tano mahakamani ili chombo hicho cha haki
kitoe tafsiri ya vitendo vya ukandamizaji wa demokrasia vinavyof… Read More
#YALIYOJIRI>>>>Diwani Chadema anaswa na dawa za kulevya, bunduki.Fahamu zaidi hapa.
Jeshi
la Polisi Mkoani Rukwa linamshikilia Diwani wa kata ya Izira, Paschael
Silimba (Chadema) baada ya kumkamata akiwa na dawa za kulevya aina ya
bangi na bunduki moja aina ya gobole.
Kamanda
wa Polisi wa mkoa huo,… Read More
Taarifa Ya Jeshi La Polisi Kwa Umma Kutoka Mkoa Wa Mwanza.Fahamu zaidi hapa.
Tarehe
12.10.2016 majira ya saa 16:35 katika eneo la Busenga “A” kata ya
Buswelu wilaya ya Ilemela jiji na mkoa wa Mwanza, askari walifanikiwa
kumkamata mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Juma Biria miaka 42,
mfanya b… Read More
0 comments:
Post a Comment