Monday 24 October 2016

BAO LA NGASSA KIVUTIO, AANZA KUONYESHA CHECHE ZAKE OMAN.FAHAMU ZAIDI HAPA.

Mshambuliaji mpya wa Fanja ya Oman, Mrisho Ngassa ameanza kuonyesha makali yake baada ya kuifungia timu yake bao katika mechi iliyochezwa mwishoni mwa wiki iliyopita.

Ngassa aliyewahi kuzichezea Yanga na Simba kwa vipindi tofauti, alifunga bao hilo akisawazisha baada ya Fanja kuwa nyuma dhidi ya Al Nah kwa bao moja, hivyo kufanya matokeo kuwa.

Hata hivyo mechi hiyo ilisha kwa sare ya mabao 2-2 lakini Ngassa akawa ameonyesha uhai mkubwa katika kikosi hicho.


Mtanzania huyo amejiunga na Fanja akitokea Free State Star ya Afrika Kusini aliyoamua kuvunja mkataba.

0 comments:

Post a Comment