Tuesday 25 October 2016

HATIMAYE NYUMBA YA KIFAHARI YA ALI KIBA YAWEKWA HADHARANI…JIKO TU LAGHARIMU MILIONI 19.FAHAMU ZAIDI HAPA.

Alikiba hajawahi kusema kuwa yupo kwenye ujenzi wa ile inayoweza kuwa nyumba ya kifahari zaidi inayomilikiwa na msanii wa Bongo.

Nyumba ya Alikiba yenye ghorofa mbili
Na sasa nyumba yake yenye ghorofa mbili imewekwa hadharani.
 Ipo maeneo ya Tabata, jijini Dar es Salaam. Picha na video za nyumba hiyo zimewekwa kwenye ukurasa mmoja wa Instagram wa shabiki wake mkubwa.
 Alikiba bado hajahamia kwenye nyumba hiyo na mafundi wanamalizia décor.
 Haijajulikana mara moja gharama ya nyumba hiyo lakini shabiki wake anadai kuwa jiko pekee limegharimu takriban shilingi milioni 19.


0 comments:

Post a Comment