Thursday 20 October 2016

#BURUDANI>>>Mr Bond Amjibu Auntylulu ' Nilipokuwa na Wewe Ulinikondosha Kwa Kero Nikawa Kama Mbuzi".Fahamu zaidi hapa.

Bond Amjibu Auntylulu kupitia Ukurasa wake wa Instagram, Ameandika haya hapa chini baada ya Aunty Lulu Kudai alimuokota jalalani, kumlea na kumtafutia kazi ya kufanya Dar es Salaam..
____
From bond_bin_sinnan 
"Dah hii dunia hii jamani, Huyu nae sijui anamuda mrefu hajatoka kwenye magazeti?
Eti Leo anafufuka na kumtukana mke Wangu eti ameniiba mimi..
Hahahaha we Lulu wewe hebu muogope mungu wako wewe. Hivi una muda gani hata sura yangu hujawahi kuiona ? Zaidi ya miaka minne hata kuniona hujawahi Leo unaanza kuleta shida kwa mke Wangu.
We siunapenda umalaya na pombe sasa zimekukifu eti ndo unaamka usingizini? Basi kama umeamka Leo fahamu tulishaachana kitambo sana na Nina mke Wangu nampenda sana anaitwa Wastara
Naomba umuache ale raha kwa uwezo wake we subiri Global wakupe kiki upate mabwana wapya.
Nilipokuwa na wewe ulinikondosha kwa kero nikawa kama mbuzi wa sadaka mpaka kuku walinikimbia. Leo mtoto wa kiarabu ananisinga nang'ara navutia mpaka unanitamani tena unifuje. Hebu niache nipumue
Maskini sijui ndo uzee unakusumbua hahahaha.. Uwiii aleyo bhagosha lelaha le pogopogo lya bhose nzogi mlyee" Ameandika Mr Bond
                                               Mr Bond na Mpenzi wake Mpya Wastara Juma

0 comments:

Post a Comment