Monday 31 October 2016

#TANZIA>>>>Bondia Thomas Mashali afariki dunia.Fahamu zaidi hapa.

Radio Free Africa kipindi cha michezo asubuhi hii wametangaza kifo cha ghafla cha Bondia Thomas Mashali. Thomas ni bondia aliyeleta changamoto kwenye gemu na kuifanya ichangamke.

Chanzo cha Kifo chake inadaiwa kuwa kimesababishwa na kipigo cha wananchi hapa maeneo ya Kimara.

Mashali aliyezaliwa kwa jina Christopher Fabian Mashale aliuawa baada ya kupigwa akiwa huko Kimara jijini Dar es Salaam. Inasemekana wakati akinywa pombe, ulizuka ugomvi na mtu mmoja ambaye anadaiwa kupiga kelele kusema Mashali ni mwizi na watu kuanza kumshambulia.

Ndugu zake wanadai kuwa walimkuta akivuja damu nyingi.

Taarifa zinadai kuwa alipelekwa katika hospitali ya Sinza Palestina kabla ya kupelekwa Muhimbili ambako mauti ilimkuta. Inasemekana kuwa hadi jioni alikuwa na bondia mwenzake, Francis Cheka.

Chanzo: Bongo5

0 comments:

Post a Comment