Monday 24 October 2016

PLUIJM AKABIDHI BARUA YA KUJIUZULU YANGA, WAMKUBALIA.FAHAMU ZAIDI HAPA.

Kocha Hans van der Pluijm ameachia ngazi rasmi kuinoa Yanga.

Pluijm ameamua kuachana na Yanga na barua yake ameikabidhi na uongozi wa Yanga tayari umemjibu.


Hii ni baada ya kamati ya Mashindano ya Yanga kuamua kumleta Kocha George Lwandamina raia Zambia.

Tayari Mzambia huyo yupo jijini Dar es Salaam akiendelea na mazungumzo na uongozi wa Yanga.

Kumekuwa na taarifa wameishamalizana lakini uongozi wa Yanga umeendelea kusema ni mazungumzo tu.

0 comments:

Post a Comment