Wednesday 4 May 2016

#YALIYOJIRI>>>SERIKALI YAIFUNGIA VIDEO YA CHURA YA MSANII SNURA,APIGWA MARUFUKU MAONESHO YAKE YA HADHARA.Fahamu zaidi hapa.

Wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo leo imetangaza kumfungia Snura kujihusisha na masuala ya sanaa ikiwemo kutumbuiza.Pia imeufungia wimbo na video yake kutochezwa kwenye redio na TV nchini.



Taarifa hiyo imetolewa mapema leo na wizara hiyo kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye ukumbi wake wa mikutano wizarani hapo.



Akiongea na waandishi wa habari, Mkuu wa Kitengo cha mawasiliano wa wizara hiyo, Zawadi Msalla, amewaonya watu kutousambaza wimbo huo kwenye mitandao ya kijamii ikiwemo WhatsApp.



Ameeleza kuwa wale watakaokiuka agizo hilo watashtakiwa kutumia sheria ya makosa ya mtandao.

Video ndo hii iliyofungiwa.

0 comments:

Post a Comment