CHAMA
 cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimepanga kulisaidia Jeshi la 
Polisi kuzuia Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Hivi
 karibuni Jeshi la Polisi lilitoa zuio la mikutano ya siasa ya wazi na 
ya ndani nchini kote, hata hivyo CCM imepanga kufanya Mkutano Mkuu 
tarehe 23 Julai mwaka huu mjini Dodoma.
Kwenye
 mkutano huo, Dk. Jakaya Kikwete, Mwenyekiti wa CCM atakabidhi mamlaka 
hayo kwa Dk. John Magufuli ikiwa ni utaratibu wa kawaida wa chama hicho.
Baraza
 la Vijana wa Chadema (Bavicha) limepanga kuzuia mkutano huo kwa madai 
ya kulisaidia Jeshi la Polisi kusimamia agizo lake kwa vyama vya siasa 
nchini.
Wakizungumza
 na waandishi wa habari jana jijini Dar es Slaam viongozi wa Bavicha 
walisema, hatua hiyo ni katika kuhakikisha wanalisaidia jeshi kutekeleza
 amri iliyotolewa na Rais Magufuli ya kuzuia mikutano ya vyama vya siasa
 hadi mwaka 2020.
“Tumeandaa
 vijana takribani 2000 kutoka mikoa yote nchini watakaokwenda Dodoma 
kusaidiana na Jeshi la Polisi kutawanya mkutano usio halali wa CCM.  Kwa
 sababau Jeshi la Polisi limezuia mikutano yote ya siasa kwa sasa.
“Pia
 ni katika kuunga mkono kauli ya Rais Magufuli kwamba, hakuna mikutano 
ya vyama vya siasa mpaka mwaka 2020. Huu ndio msiamamo wa baraza.
“Mikutano
 yetu sisi kama Chadema tunazuiwa lakini CCM wanafanya. Mahafari ya 
chama cha mapinduzi yanafanyika. Ni jana CHASO (Jumuiya ya Wanafunzi wa 
Vyuo Vikuu Chadema) Morogoro tumezuiwa lakini UVCCM (Umoja wa Vijana wa 
CCM) Mkoa wa Morogogo wamefanya na picha zipo. Hii sio haki, kama mbwai 
na iwe mbwai,” alisema Patrick ole Sosopi, Makamu Mwenyekiti wa baraza hilo.
George Tito, Mwenyekiti wa Bavicha Mkoa wa Mbeya alisema “… ni kwamba, huko mikoani vijana wameshajipanga. Wana ari kubwa ya kwenda Dodoma.
“Tumeamua
 kufikia hatua hii kwa sababu tumekuwa tunaona hakuna haki katika nchi 
hii. Kuna mahafali yanafanyika vyuo vikuu, wenzetu CCM wanaruhusiwa sisi
 Chadema tunakatazwa.Vijana wa Chadema wamekuwa wakikamatwa bila sababu 
za msingi,” alisema Tito.













0 comments:
Post a Comment