Dully Sykes amedai kitendo chake cha kubadilisha muziki kutoka kwenye
Hip Hop mpaka kwenye kuimba kulifanya baadhi ya wasanii wenzake
kumchukia.
Muimbaji huyo ni mmoja kati wa wasanii
wachache wapo muda mrefu kwenye tasnia ya muziki ikiwa ni zaidi ya miaka
15 lakini mpaka leo hii anaendelea kufanya vizuri kwa kuachia hit kibao
na kuwatoa jasho wasanii walioanza kufanya muziki hivi karibuni.
“Watu wa Hip Hop walinipiga sana vita
mpaka ikafikia wakati rafiki zangu wakanichana kidogo wakina mwana FA na
Jay Moe,” ameiambia BBC.
Wimbo ambao Dully anadai kuwa alichanwa
na wasanii haoni ‘Ingekuwa Vipi’ ambao jina lake limetajwa ndani ya
wimbo huo japo siyo peke yake aliyetajwa.
“Ingekuwa vipi Dully Sykes angeimba
hardcore mashairi kama Jay Moe neno wanasesere nina imani
lisingekuwepo,” Mwana FA anarap kwenye Ingekuwa Vipi.
Kwa sasa msanii huyo anafanya vizuri na
wimbo wake wa ‘Inde’ aliomshirikisha Harmonize ambao umefanikiwa
kutazamwa kwa zaidi ya milioni 1 na laki 2 ndani ya wiki tatu kwenye
mtandao wa YouTube.
0 comments:
Post a Comment