Saturday 3 September 2016

#MICHEZO>>>STARS YAUMIZWA NA NIGERIA.FAAMU ZAIDI HAPA.

Goli pekee la kika ya 76 la mshambuliaji wa Manchester City Kelechi Iheanacho limeendeleza rekodi ya Stars kushindwa kupata ushindi mbele ya Nigeria ambapo kwa mujibu wa rekodi, Stars haijafanikiwa kupata ushindi ushindi mbele ya The Super Eagles tangu timu hizo zilipoanza kukutana.

Stars ilisafiri hadi Nigeria kwenda kucheza mchezo wa kukamilisha ratiba katika Kundi G ikiwa ni mechi ya kutafuta nafasi ya kufuzu kucheza fainali za michuano ya mataifa ya Afrika (AFCON 2017) nchini Gabon.

Hadi hatua ya makundi inamalizika, Stars haijafanikiwa kupata ushindi katika Kundi G baada ya Chad kujitoa kwenye kundi hilo kutokana na matatizo ya kifedha. Ushindi pekee wa Tanzania ulikuwa ni dhidi ya Chad ambapo Stars ilipata ushindi wa goli 1-0 ugenini lakini ushindi huo ulifutwa baada ya Chad kujiengua.

0 comments:

Post a Comment