Tuesday 11 April 2017

Yaani Hata CCM Wamshangaa Roma... Wahoji Anaficha Nini.Fahamu zaidi hapa.

Na Thadei Ole Mushi.
Kutokana na Maelezo ya Roma na kutekwa kwake ni kwamba hajui waliomteka na wala hajui watekaji walikuwa wanahitaji nini.
Maswali ninayojiuliza....
#Roma anadai hajui kwa nini alitekwa ila anasema watekaji walipomchukua walienda kumhoji. Kama walimhoji moja kwa moja anawajua waliomteka. 
Aidha walimhoji kumuuliza labda kama anatembea na mke wa mtu, au walimhoji kuhusu kujihusisha na siasa, au walimhoji kuhusu nini??
Kutokana na mahojiano hayo moja kwa moja Roma anajua waliomteka ni kina nani kama hawajui atuambie walimuuliza maswali gani tutamsaidia kumwambia ni kina nani hao au na sisi tutaridhika kuwa kwa kweli maswali hayo yalikuwa hayaeleweki. 
Sitaki kuongea sana hili naweza kuvuka mipaka na kuzidi kuuweka ukweli upenuni.
#Raia wa Tanzania wana ulinzi kiasi Gani??? Kutokana na Issue hii??? Yaani mtu anatekwa na simu yake ipo hewani na sms anasoma ila bado polisi wetu hawajui alipo mtu huyo. Kama haya yanaweza kufanyika jeshi letu halioni linajiondolea weledi mbele ya raia? 
Mtu anatekwa Studio taarifa zinafikishwa polisi gari waliyoondoka nayo inajulikana ni Noah na hata number za Gari zitakuwa zinajulikana ila bado polisi wanashindwa kusema ni kina nani hao.... 
Ubaya mmoja haya mambo hayafuatiliwi na watanzania tu bali hata majirani zetu hamuoni mnawakaribisha wakidhani mu dhaifu kwenye maswala ya kiulinzi?
#TongweRecords hawana Mlinzi? Kama wanaye walimteka na yeye?? Maana kipengele hiki wamekisahau kwenye hili Tukio. Kama Mlinzi alikuwepo alikubalije watu kuingia ndani ya Studio na kuondoka na vitu? Je walipoingia Getini hawakujiandkisha?????
#Waliotekwa ni wanne kwa nn Roma aende peke yake kujieleza? Katika wote waliotekwa yeye ndiye aliyepigwa zaidi kwa maelezo yake kwa nn hao wengine hawakumsaidia kwenda kuongea na vyombo vya habari wakati yeye akiendelea kujiuguza?
Hawaoni kuwa kwa tafsiri ya kawaida kabisa watakayoipata wananchi ni kuwa kama wangeenda wote wangejichanganya kimaelezo? Tayari kina Roma wanajua kuwa mtaani kuna sintofahamu kuhusu wao hawaoni kuwa kwa kutokufika wote kutaruhusu wazo hili na kuongeza hii sintofahamu??
#Roma anadai kuwa walitupwa karibu na dimbwi wakajikokota wakapakia pikipiki wakaenda nyumbani kubadili nguo. Ila walipofika nyumbani hawakumkuta mtu hivyo walilazimika kuvunja mlango....
Ni boda boda gani iliwachukua toka hapo walipotupwa?? 
Roma bado alikuwa na simu yake kwa nini avunje mlango badala ya kumtafuta mkewe kwenye simu ili aje kumfungulia mlango?
Kama walimnyanganya simu ni kweli kuwa alikuwa hajui simu ya mkewe?? Si angelitafuta simu mahali ampigie?
Je majirani wa kina Roma ni nani walisikia vishindo vya kuvunja mlango?? 
Na kama walisikia walichukua hatua Gani?.........
#Hata eye contact ya Roma ina Mashaka asilimia 90 kashindwa kuamgalia waandishi anajishika usoni tena machoni. Wala hakuwa na hisia za mtu ambaye kweli alitekwa.
#Unatekwa unateswa unaumizwa halafu unaenda nyumbani kubadili nguo..... Si unapoteza ushahidi?? Kwa nn aende Polisi akiwa ameshabadili nguo? 
Sitaki uamini kama ninavyoamini tuendelee na story zetu za kawaida........nilishasema hutakiwi kufikiri sana ukiwa Tanzania.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment