Monday 20 July 2015

#Breaking news>>Burundi milipuko yashamili.


Kumetokea ufyatulianaji wa risasi na milipuko usiku kucha nchini Burundi, usiku wa kuamkia uchaguzi wa rais uliozua utata. Kiongozi wa sasa wa nchi hiyo anawania muhula wa 3 kama rais licha ya madai kuwa anakwenda kinyume na katiba ya nchi.
Viongozi wengi wa upande wa upinzani wameapa kususia uchaguzi huo.
Saa chache tu kabla ya kufunguliwa shughuli ya upigaji kura, milipuko ya gruneti iliripotiwa jijini Bujumbura na kufuatiwa na milio ya risasi. Maeneo mengine risasi hizo zilisikika kwa wingi zaidi mjini humo. Japo haikuwa wazi ni nani hasa anayefyatua risasi hizo.
Kwa mujibu wa mshauri wa kisasa wa rais, haya ni mashambulio yanayofanywa na 'magaidi' wanaonuia kuvuruga shughuli ya uchaguzi.
 Chanzo
                 BBC Habari.

0 comments:

Post a Comment