Thursday 21 April 2016

BREAKING NEWS>>>>KATIBU MKUU WA ACT WAZALENDO SAMSONI Mwigamba abwaga manyanga.Fahamu zaidi hapa.

Katibu Mkuu wa Chama cha ACT - Wazalendo, Samson Mwigamba 

Dar es Salaam. Katibu Mkuu wa Chama cha ACT - Wazalendo, Samson Mwigamba amejiuzulu nafasi yake ilia pate nafasi ya kwenda masomoni Chuo Kikuu cha Kenyatta nchini Kenya.

Kwa mujibu wa ACT-Wazalendo, kamati ya uongozi imekubali maombi ya Mwigamba na kumruhusu kwenda masomoni na kuwa mchakato wa kujaza nafasi hiyo utaanza mara moja.

Naye Mwigamba ameushukuru uongozi wa chama chjake kwa ushirikiano waliompatia tangu chama hicho kinaanzishwa. Amesisitiza kwamba bado ni mwanachama na ataendelea kutoa ushirikiano hata akiwa nje ya nchi.

Mwanasiasa huyo anakwenda kusoma shahada ya uzamili katika masuala ya utawala na usimamizi wa biashara (MBA) na baada ya masomo hayo ataendelea na shahada ya uzamivu (PhD)

0 comments:

Post a Comment