Monday 18 April 2016

RONALDO AMEAMUA KUTULIA KWA KIFAA CHA KI-AFRIKA.FAHAMU ZAIDI HAPA.

Cristiano Ronaldo sasa anahusishwa na mrembo mwingine wa Angola Maria Borges baada ya awali kutoka taarifa kwamba anatoka na model wa kituruki Cansu Taskin ambaye alifanyiwa mahojiano na kituo kimoja cha television na kumwagika kila kitu kuhusu uhusiano wake wa kimapenzi na superstar huyo wa Ureno.

Picha kadhaa zinasambaa kwenye mitandao ya kijamii zikimuonesha Cristiano Ronaldo akipata dinner na mrembo Maria Borges ambaye ni model.
Tukio hilo limetokea wiki iliyopita wakati Ronaldo na Maria Borges walipoungana group kubwa la watu kupata chakula.
Kwa mujibu wa ripoti, mtoko huo kwa ajili ya dinner ulifanyikia Paris usiku ambao Ronaldo alipiga hat-trick kwenye Champions League Real Madrid ilipoishinda Wolfsburg kwa magoli 3-0 na kufuzu kucheza hatua ya nusu fainali ya michuano hiyo.
Madrid imepangwa na Manchester kwenye nusu fainali ya Champions League baada ya Man City kubwaga PSG kwenye hatua ya robo fainali.

Los Blancos walirejea tena uwanjani Jumamosi na kutoa kichapo cha bao 5-1 ugenini dhidi ya Getafe kwenye mchezo wa La Liga.

0 comments:

Post a Comment