Friday 29 April 2016

#MICHEZO>>>FARID MUSA TAYARI KAPIMWA AFYA, ATASAINI DEAL SPAIN.Fahamu zaidi hapa.

 Habari njema kuhusu winger wa Azam FC na timu ya taifa ya Tanzania Farid Musa ni kwamba, leo amefanyiwa vipimo vya afya ili kujua ufiti wake, Tenerife wamesema ikiwa atafanikiwa kufaulu vipimo hivyo, wangependa wamchukue kwa mkopo wa miaka miwili (2).
 Farid Musa ameongezewa wiki moja nyingine ya majaribio na Club Deportive Tenerife ya nchini Hispania ambako ameenda kusaka mafanikio ya soka la kulipwa nje ya Tanzania.
Yusuf Bakhresa ambaye yuko pamoja na Farid nchini Hispania, ameiambia www.shaffihdauda.co.tz kwamba inavyoonekana mpaka sasa Farid ananafasi kubwa ya kubaki kwenye klabu hiyo.

0 comments:

Post a Comment