Thursday 21 April 2016

RASMI YANGA YAPANGWA NA TIMU KUTOKA ANGOLA KATIKA CAF .FAHAMU ZAIDI HAPA.

Baada ya Yanga kufungwa mabao 2-1 na Al Ahly ya Misri na hivyo kutolewa katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa jumla ya mabao 3-2, timu hiyo ya Jangwani sasa imepangiwa timu kutoka Angola katika Kombe la Shirikisho hatua ya mtoano.

Kanuni za Shirikisho la Soka la Afrika (Caf) zinaeleza kuwa timu ambazo zitatolewa katika Raundi ya Pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika zitashuka katika Kombe la Shirikisho ambapo huko zitakutana na timu nane zilizosonga mbele ambapo zitacheza mechi za mtoano za nyumbani na ugenini kisha zitakazofuzu zitaingia hatua ya makundi.

Baada ya Yanga kutolewa, sasa itakutana na Sagrada Esperança baada ya droo kupangwa jana huku Yanga ikitakiwa kuanzia nyumbani wiki ya Mei 6-8, mwaka huu na marudio ni Mei 17-18, 2016.

RATIBA KAMILI YA MTOANO KOMBE LA SHIRIKISHO IPO HIVI: 


MO Béjaïa (Algeria)     Vs     (Tunisia) Espérance de Tunis Stade Malien (Mali)    Vs        (Morocco) FUS Rabat
Étoile du Sahel (Tunisia)     Vs    (Gabon) CF Mounana
TP Mazembe (DR Congo)     Vs    (Tunisia) Stade Gabèsien
Al-Ahli Tripoli (Libya) Vs         (Misri) Misr El-Makasa
Al-Merrikh (Sudan)     Vs    (Morocco) Kawkab Marrakech
Young Africans (Tanzania)     Vs    (Angola) Sagrada Esperança
Mamelodi Sundowns (Sauz) Vs     (Ghana) Medeama

0 comments:

Post a Comment