Thursday 6 October 2016

#BURUDANI>>>Saida Karoli " Nilitumiwa, Ukiona Ninapoishi Utasikitika.Fahamu zaidi hapa.

Saida Karoli anaogopa kugusa hata jani, akidhani
ni nyoka anayetaka kumng’ata

Ni kwasababu licha ya kufanya vizuri kimuziki
miaka kadhaa iliyopita, hakupata chochote na
bado anaishi katika mazingira magumu.
 
“Niliumizwa kuanzia mwanzo, ni vitu vichache
nilivyovipata, kama mkibahatika waandishi wa
habari wenye makamera na wakija kwangu
watashuti kulingana na nilivyo, wataona
mazingira ninayoishi ndipo watanzania watazidi
kufunguka zaidi,” Saida alimwambia mtangazaji
wa Jembe FM, Natty E.
 
Kwa sasa Saida Karoli anaishi jijini Mwanza. Hivi
karibuni amerejea tena kwenye midomo ya watu
baada ya Diamond kurudia wimbo wake Salome.

0 comments:

Post a Comment