Wakati vyuo vikuu vikikaribia kufunguliwa, Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imelaumiwa kwa kuchelewa kutoa majina ya wanufaika huku yenyewe ikisema itahakikisha majina yanatolewa sanjali na tarehe za vyuo kufunguliwa.
Pia, HESLB imesema miongoni mwa vipaumbele vitakavyozingatiwa kwenye utoaji wa mikopo katika mwaka wa masomo 2016/2017 ni kwa wanafunzi wenye mahitaji makubwa, waliotoka kwenye kaya masikini, waliosoma shule za kata na waliotoka vijijini. 
Kauli
 hiyo imekuja baada ya bodi hiyo kutupiwa lawama kwa kuchelewa kutoa 
majina ya wanufaika wa mikopo kabla hawajaripoti vyuoni, hasa wanafunzi 
wa mwaka wa kwanza.
Mkurugenzi
 wa mtandao wa haki za wanafunzi (TSNP), Shitindi Venance alisema hadi 
sasa wanafunzi wanaojiunga na masomo ya elimu ya juu nchini kwa mwaka wa
 kwanza wa masomo 2016/2017, ambao wameomba mkopo bado hawajui ni kiasi 
gani wamepewa. 
Malalamiko
 ya Shitindi yamerejea kilichotokea mwaka jana baada ya wanafunzi 
kuripoti vyuoni, lakini majina yalipotolewa na bodi hiyo baadhi yao 
hawakuwa wanu- faika hali iliyosababisha usumbufu. 
Mkurugenzi
 Mtendaji wa HESLB, Abdul-Razaq Badru alisema miongozo ya utoaji wa 
mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu kwa mwaka huu ni tofauti na mwaka 
jana. 
“Utaratibu
 wa mwaka huu ni tofauti kwa kuzingatia wanafunzi wanaoanza masomo na 
wale wanaoendelea na masomo katika vyuo mbalimbali,” alisema Badru. 
Mkurugenzi
 huyo alibainisha kuwa majina ya wanufaika wa mikopo yataanza kutolewa 
kwa kuzingatia tarehe ambayo chuo husika kinafunguliwa.
 “Kila
 chuo kinafunguliwa kwa mujibu wa tarehe iliyopangwa kwa hiyo na sisi 
tunatoa majina kuendana na utaratibu wa chuo husika,” alisema. 
Hata
 hivyo, Badru alisema uta- ratibu wa kupanga viwango vya mikopo kwa 
wanafunzi na kisha kutoa orodha ya majina ya wanufaika haihusishi bodi 
ya mikopo peke yake. 
Alisema
 kabla ya kuidhinisha majina ya wanufaika na mikopo, lazima Tume ya Vyuo
 Vikuu Tanzania (TCU) iwe imeshatoa orodha ya majina wa wanafunzi ambao 
imewadahili kwa kuzingatia vigezo vyao, halafu majina hayo yatumwe 
vyuoni. 
Alisema mzunguko wote huo unahitaji muda na umakini wa hali ya juu ndiyo maana huchukua muda. 












0 comments:
Post a Comment