Tuesday 27 June 2017

HATIMAYE..Rayvanny Akamilisha Ndoto yake Kwa Jason Derulo.

Kushindwa kutumia fursa kwa kila nafasi unayoipata imeonekana ni dhambi kubwa kwa wasanii wa WCB. Hatimaye Rayvanny amekamilisha ndoto yake aliokuwa akiiota kwa muda mrefu.


Hitmaker huyo wa Zezeta, ambaye siku chache zilizopita alinyakuwa tuzo ya BET, amefanikiwa kukamilisha kufanya kazi na Jason Derulo kutoka Marekani.

Kupitia mtandao wa Instagram, Ray ameweka picha akiwa syudio na msanii huyo na kuandika, “God bless you my brother @jasonderulo its amaizing opportunity,am so grateful for that……… Toka Saa 8 Usiku amekaa na mimi hadi Asubui… Studio kulikua na Watoto wakaaaaaliiiii 😂lakini kawacha waondoke sababu walichoka kukaa studio yeye kabaki na sisi tu. Naamini kilichofanyika Mtakipenda. Thanks boss @afrikidd @babutale.”

Baada ya wasanii hao kukamilisha kazi yao hiyo walijumuika pamoja katika kucheza mchezo wa mpira wa kikapu ambapo Ray alijikuta akiambulia za uso kutoka kwa Jason. Wawili hao kwa mara ya kwanza walikutana nchini Kenya kwenye Coke Studio Afrika wiki chache zilizopita.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment