Friday 30 June 2017

Meya wa Ubungo Dsm, Amefanya Uzinduzi Huu Jana.

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ubungo, Boniface Jacob, leo Ijumaa 30 Julai 2017, amezindua kituo cha kisasa cha kukusanya kodi, ushuru na tozo mbalimbali katika eneo la Simu 2000 pamoja na Kuhamsisha wafanyabiashara,bodaboda na Abiria wa Mabasi madogo .

Hii itapunguza kero kwa  wananchi wanaoishi maeneo ya karibu na eneo la Simu 2000, kulipa kodi, ushuru na tozo mbalimbali ambapo awali walilazimika kwenda Kibamba zilizopo ofisi za Manispaa ya Halmashauri ya Ubungo.

Kituo hiki kipya kinategemea kuwasaidia wakazi wa Sinza, Makurumla, Mburahati, Mabibo, Makuburi, Ubungo na maeneo yote ya karibu.

Aidha amewataka Halmashauri ya Ubungo, kuwalinda na kuwatetea Bodaboda dhidi ya TANROADS na JESHI LA POLISI kwa kusajili vituo vya kupaki pikipiki na bajaji na kuwapa namba za utambuzi kwakuwa Bajeti ya Halmashauri 2017/218, inawategemea kuwapatia Bodaboda na Bajaji kiasi cha shillingi Billioni 4 kama chanzo cha mapato.Wakiendelea kughasiwa Halmashauri itazikosa pesa hizo.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment