Sunday 25 June 2017

Saida Karoli: ‘Urugambo’ inanikumbusha mpenzi wangu.

Mwanamuziki mkongwe wa nyimbo za asili, Saida Kalori, ambaye kwasasa anatamba na wimbo wake mpya ‘Urugambo’ ametoa ya moyoni kuwa wimbo huo unamkumbusha mpenzi wake wa zamani.

Saida anasema umaarufu wa wimbo huo umemsababishia kero kwa midume wakware ambao kila kukicha wanampigia simu.

Hata hivyo Saida amesema hataki kuwasikia kwani amechoshwa na tabia za wanaume wanaomfuata kwa malengo yao kisha humtema mara wanapofanikiwa malengo yao.

Alisema ni bora amtafute mpenzi wake wa zamani ambaye kila anapomfikiria anaumia kutokana na mapenzi mazito aliyonayo kwake.

Saida alianza kuwa maarufu miaka ya mwanzao ya 2000, baada wimbo wake ‘Salome’ kuwa maarufu ndani na nje ya nchi.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment