Friday 30 June 2017

Msanii Bobi Wine Ashinda Ubunge Nchini Uganda.

Msanii wa muziki kutoka nchini Uganda, Robert Kyagulanyi Ssentamu almaarufu kama, Bobi Wine ameshinda ubunge katika uchaguzi mdogo nchini humo.

Tokeo la picha la bobi wine
Bobi Wine mwenye suti katikati akikabiliana na Askari Polisi mapema wiki hii

Wine, ambaye aliwania kama mgombea huru, aliwashinda wagombea wenzake wanne katika jimbo la Kyadondo Mashariki mwa Uganda kwa ushindi wa kura 25,659 kati ya kura elfu  33,310 zilizopigwa.

Kwa mujibu wa Gazeti la New Vision la nchini humo limeeleza kuwa baada ya kutangazwa Gazeti hilo linasema baada ya kutangazwa kuwa mshindi, aliahidi kurudisha umoja na mshikamano jimboni humo.

“Jambo langu la kwanza ninalotaka kufanya ni kufanikisha maridhiano kati ya viongozi wa Kyadondo Mashariki…Ninataka siasa zitulete pamoja… jinsi muziki ufanyavyo.“amesema Bob Wine.

Mwanamuziki huyo mapema wiki hii alikamatwa na polisi na kuhojiwa kwa muda kabla ya kuachiwa huru.

Kiti hicho cha ubunge kiliachwa wazi baada ya mahakama kufuta matokeo ya uchaguzi huo kwa madai kuwa uchaguzi huo haukuwa huru na wa haki.

Kiongozi wa chama cha upinzani cha FDC Kizza Besigye amempongeza mwanamuziki huyo kwenye kupitia ukurasa wake wa Twitter.


obi Wine alianza muziki mapema miaka ya 2000 kabla ya kujitosa kwenye siasa uchaguzi mkuu mwaka 2016 na ngoma ambayo ilimfanya ajizolee umaarufu nchini humo ni wimbo wake wa Situka.

Kwenye wimbo huo, anatoa wito kwa raia wa Uganda kuchangia katika vita dhidi ya rushwa na ukiukaji wa haki nchini mwao.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment