Saturday 14 May 2016

#MICHEZO>>>KUTANA NA MABUSU MANNE NDANI YA UWANJA YALIYOWAHI KUIBUA HISIA TOFAUTI.Fahamu zaidi hapa.

Kila mtu anafahamu fika kuwa busu si kitu kigeni katika mazingira ya ulimwengu wa sasa na hata zamani pia. Watu hufanya hivi kuonesha mapenzi ya dhati kwa wenzi wao ama kufikisha ujumbe fulani.

Katika mchezo wa mpira wa miguu, mara nyingi tunaona wachezaji wakiwabusu ama wake zao au wapenzi wao na vitu kama hivyo.

Lakini kuna matukio yasiyo ya kawaida ambapo tumeshuhudia wachezaji wakibusiana wenyewe kwa wenyewe . Haya ndio matukio manne ambayo yalileta hisia zisizo za kawaid akatika ulimwengu wa soka.

4. Busu la Messi dhidi ya Alba

Hii ilitokea wakati Messi alipofunga goli zuri na ndipo Jordi Alba aliopjikuta anapiga busu zito bila kujua huku Messi kwa upande wake akilipokea pia bila ajizi. Wakati mwingine mchezo wa mpira wa miguu ni mzuri sana.
  1. Busu la Debuchy dhidi ya Giroud

wakiwa timu ya taifa na kufunga goli maridadi. Baada ya goli hilo wawili hao walijikuta wakipigana busu zito kwa furaha bila ya kujali kitendo hicho kingezua mjadala machoni mwa watu.

2.Busu la Gerrard dhidi Alonso
Hii ilikuwa wakati wa fainali ya Klabu Bingwa barani Ulaya wakati Liverpool wakitoka nyuma kwa mabao matatu na kurudisha yote dhidi ya AC Milan mwaka 2005 jijini Istanbul. Baada ya ushindi wa penati nahodha Steven Gerrard na kiungo mwenza Xabi Alonso walichagua staili ya aina yake ya kushangilia kwa kupigana busu na kugonga vichwa vya habari vya media nyingi ulimwenguni.
  1. Busu la Gary Neville dhidi ya Paul Scholes
‘Malegend’ hawa wawili wa Man United walijikuta wakipigana busu zito bila ya kujua kutokana na furaha nzito waliyokuwa nayo baada ya Paul Scholes kufunga goli murua dhidi ya mahasimu wao wakubwa wa Ligi ya England Manchester City.

0 comments:

Post a Comment