Wednesday 28 December 2016

Haya ndio majibu ya mchezaji wa Simba, Ibrahim Hajib baada ya kufanya majiribio Misri.Fahamu zaidi hapa.

Mchezaji wa kimataifa wa Tanzania na klabu ya Simba, Ibrahim Hajib ambaye hivi karibuni alienda Nchini Misri kufanya majaribio katika klabu ya Haras El Hodoud ya Ligi Kuu ya Misri.

Hajib (kushoto) akiwa na wachezaji wenzake wa Haras El Hodoud mazoezini leo mjini Alexandria
Hajib akiongea na Bin Zubeiry Sports kutoka mjini Alexandria yalipo makao makuu ya timu hiyo, Hajib alisema kwamba ameambiwa amefuzu majaribio yake baada ya siku tano.
“Nimepewa majibu kwamba nimefuzu, kwa hiyo kinachofuata ni hii klabu kuzungumza na Simba ili wakubaliane kwanza, ndipo nitajua mustakabali wangu,”amesema Hajib.
Hajib ambaye aliondoka Alhamisi iliyopita nchini kwenda Misri kwa majaribio ya kucheza soka ya kulipwa baada ya kupewa baraka zote na uongozi wa Simba.
Source: Bin Zubeiry Sports

Download  Application ya Hebron Male Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi


Bonyeza Hapa CLICK HERE

                              Follow me instagram 

 

0 comments:

Post a Comment