Saturday 18 June 2016

#YALIYOJIRI>>>Kauli ya TCRA katika mchakato endelevu wa kuzima simu feki.Fahamu zaidi hapa.

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Innocent Mungy amesema kuwa mtambo wa kuzima simu bandia unaendelea na kazi kuhakikisha kuwa hata simu ambazo hazikuwa hewani zitakapowashwa hazitafanya.
Alisema kuwa simu feki ambazo hazikuwa hewani usiku wa kuamkia juzi zitakapowasha hazitafanya kazi kwa kuwa mtambo wa kuzima Imei bandia unaendelea kuhakiki simu hizo.

Mkurugenzi wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Innocent Mungy amesema jana kuwa mtambo wa kuzima simu bandia unaendelea na kazi kuhakikisha kuwa hata simu ambazo hazikuwa hewani zitakapowashwa hazitafanya.

Kazi ya kuzima simu hizo ilianza usiku kumkia juzi saa sita usiku na kila kampuni ya mtandao wa simu ilipaswa kuzima simu za wateja wake ambazo ni feki na kazi ya mtambo ni kuhakikisha simu iliyozimwa inapowekewa kadi ya mtandao mwingine haifanyi kazi na kuhakikisha simu zote feki zitakazoingia nchini hazifanyi kazi,” amesema Mungy.

Baadhi ya wananchi waliozimiwa simu wameilalamikia Serikali kwa kuwasababishia hasara kwa madai ya kutokuwa makini katika kudhibiti uingizwaji wa bidhaa feki.

Pendo Mpomelo, mkazi wa Kimara jijini Dar es Salaam alisema simu yake ilikosa mawasiliano kuanzia saa saba usiku

Source: Mwananchi

0 comments:

Post a Comment