Saturday 18 June 2016

Mwasiti kuachia ngoma mpya aliyomshirikisha Chidi Benz.Fahamu zaidi hapa.

Mwasiti anatarajia kuachia ngoma mpya aliyomshirikisha rapper huyo. Amesema huo ni wimbo waliofanya kitambo lakini ulikuwa bado kwenye makabati.

Akiongea na 255 ya XXL kupitia Clouds FM, Mwasiti amesema wimbo huo uliorekodiwa miaka miwili iliyopita unaitwaWanipa Raha’ na kwamba ni bonge la ngoma. “Ni kazi nzuri ambayo huwezi kusema imerekodiwa miaka miwili au mitatu iliyopita utasema ni ngoma ambayo imerekodiwa jana labda kwasababu ni kazi nzuri sana,” amesema Mwasiti.

Amesema wimbo huo umetayarishwa na Tudd Thomas.
Mashabiki wengi wameimiss sauti ya Chidi ambaye hivi karibuni alipelekewa Bagamoyo kwenye kituo cha kusaidiwa waathirika wa madawa ya kulevya.

0 comments:

Post a Comment