Saturday 25 June 2016

#MICHEZO>>>>KESSY ATACHEZA DHIDI YA MAZEMBE? TFF IMETOA UFAFANUZI.Fahamu zaidi hapa.

Shirikisho la mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kupitia msemaji wake, Alfred Lucas limesema kuwa, linashughulikia sakata la uhamisho wa mchezaji Hassan Kessy Ramadhani kutoka Simba kwenda Yanga ili aweze kucheza kwenye mchezo wa kimataifa kati ya Yanga dhidi ya TP Mazembe unaotarajiwa kuchezwa siku ya Jumanne June 28 kwenye uwanja wa taifa.

“Tayari Yanga wameshaandika barua imekuja TFF wakiomba suala la Kessy liweze kumalizwa haraka ili waweze kumtumia kwenye mchezo wao wa Jumanne dhidi ya TP Mazembe,”amesema Alfred Lucas afisa habari wa shirikisho la soka Tanzania.

“Niwahakikishie mashabiki wa Yanga kwamba TFF weekend yote hii kwa maana ya leo Jumamosi na Jumapili tutalifanyia kazi hilo na tayari mawasiliano yameshafanyika ili Yanga waanze kumtumia mchezaji huyu mara baada ya mkataba wake kuisha.”

“Lakini kama kuna kikwazo chochote tunajaribu kufikiria ili Yanaga wawe huru kusiwe na dosari yeyote kwenye michuano hii halafu sababu ikawa ni kuwakosa wachezaji wake wote iliyowasajili kwa ajili ya michuano hiyo.”

“Naamini kwa uungwana waliokuwa nao Simba kama kuna kikwazo watakiondoa ili mchezaji huyo aendelee kipaji chake na maisha mengine yaendelee.”

Kessy hakuruhusiwa kucheza kwenye mchezo wa kimataifa kati ya Yanga dhidi ya MO Bejaia kwasababu kibali chake kutoka Simba kwenda Yanga kilikuwa hakijathibishwa.

0 comments:

Post a Comment