Siku nne zimepita tangu Hitmaker wa
Mabawa Msamibaby atimize miaka 27, ambapo amekutana na suprise kubwa
kutoka kwa menejimenti yake ambayo imemzawadia gari aina ya Toyota Ipsum
yenye thamani ya shilingi milioni 15, jambo ambalo amelipokea kwa
shangwe za kutosha kwani ilikuwa kinyume na matarajio yake.
Meneja wa
Msanii Rehema Jonas maarufu kama Reyjons amesema wameamua kumpatia gari
hiyo aina ya Toyota Ipsum kama zawadi ya Birthday kwa kutambua umuhimu
wa siku hiyo kwake.
Katika makabidhiano hayo ya gari kati ya
msami na menejimenti yake jambo ambalo limeibua hisia tofauti ni uwepo
wa msanii Kajala katika hafla hiyo fupi na kutilia hofu huenda kuna
jambo linaendelea kati ya mastaa hao wawili ambapo msami amefunguka
zaidi kuhusu hilo kwenye Audio hapo chini.
0 comments:
Post a Comment