Saturday 11 June 2016

#BURUDANI>>>BAADA YA KUZAWADIWA GARI MSAMI AFUNGUKA MAHUSIANO YAKE NA KAJALA(+Audio).Fahamu zaidi hapa.

Siku nne zimepita tangu Hitmaker wa Mabawa Msamibaby atimize miaka 27, ambapo amekutana na suprise kubwa kutoka kwa menejimenti yake ambayo imemzawadia gari aina ya Toyota Ipsum yenye thamani ya shilingi milioni 15, jambo ambalo amelipokea kwa shangwe za kutosha kwani ilikuwa kinyume na matarajio yake.

 
Meneja wa Msanii Rehema Jonas maarufu kama Reyjons amesema wameamua kumpatia gari hiyo aina ya Toyota Ipsum kama zawadi ya Birthday kwa kutambua umuhimu wa siku hiyo kwake.
 
Katika makabidhiano hayo ya gari kati ya msami na menejimenti yake jambo ambalo limeibua hisia tofauti ni uwepo wa msanii Kajala katika hafla hiyo fupi na kutilia hofu huenda kuna jambo linaendelea kati ya mastaa hao wawili ambapo msami amefunguka zaidi kuhusu hilo kwenye Audio hapo chini.




0 comments:

Post a Comment