Home »
Michezo
» DUNGA ATIMULIWA BRAZIL BAADA YA KUTIA AIBU COPA AMERICA.Fahamu zaidi hapa.
Dunga amefutwa kazi kama kocha mkuu wa Brazil baada ya kuondoshwa kwenye michuano ya Copa Amerika katika hatua ya makundi.
Dunga ambaye alikuwa nahodha aliyepata mafanikio akiwa na Brazil kwa
kuiwezesha kutwaa kombe la Dunia mwaka 1994, alitangazwa kuwa kocha wa
timu ya taifa kwa mara ya pili mwaka 2014.
Kikosi cha Brazil kilifungashiwa virago kwenye hatua ya makundi ya
michuano ya Copa America kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1987 baada ya
kuchezea kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Peru siku ya Jumapili.
Dunga, 52, mara ya kwanza alikuwa kocha wa Brazil kuanzia mwaka 2006
hadi 2010, akafanikiwa kushinda taji la Copa America mwaka 2007.
Kocha wa klabu ya Corinthians anapewa nafasi kubwa ya kurithi nafasi iliyoachwa wazi na Dunga.
Kocha huyo mwenye miaka 55 alikiongoza klabu hiyo kushinda taji la
ligi kuu ya Brazil (Serie A) mwaka 2011 na 2015, pamoja na Copa
Libertadores na World Club Cup mwaka 2012.
Hata hivyo, kocha atakayemrithi Dunga atakiongoza kikosi cha Brazil
cha U23 kikiwa na nyota wa Barcelona Neymar kupambana kwenye michuano ya
Olympic itakayofanyina Rio de Janeiro, Brazil kuanzia mwezi August.
Mrithi wa Dunga pia atakuwa kwenye wakati mgumu kuhakikisha Brazil
inafuzu kucheza kombe la dunia nchini Russia mwaka 2018 kutokana na
mwendo wa kusuasua wa kikosi hicho kinachokamata nafasi ya sita kwenye
kundi lake katika mbio za kufuzu kwa fainali hizo.
Related Posts:
#MICHEZO>>>CHRIS SMALLING ANGA’NG’ANIWA VIPIMO VYA MADAWA UHOLANZI, POLISI WAINGILIA KATI.FAHAMU ZAIDI HAPA.
Beki
wa Manchester United, Chris Smalling, usiku wa jana alilazimika kupata
msaada wa polisi wakati akielekea uwanja wa ndege baada ya mchezo wa
timu yake dhidi ya Feyenoord katika Europa League nchini Uholanzi.
S… Read More
#MICHEZO>>>>MABADILIKO MENGINE LIGI KUU BARA, SIMBA, YANGA VIWANJANI WIKIENDI HII.FAHAMU ZAIDI HAPA.Ligi
Kuu ya Tanzania Bara msimu wa 2016/2017 inatarajiwa kuendelea Jumamosi
na Jumapili hii lakini kuna mabadiliko ya mchezo mmoja uliotakiwa
kuchezwa Jumapili sasa utachezwa Jumanne. Mabadiliko hayo ni mwendelezo
wa Shir… Read More
#MICHEZO>>>Wapiganaji wapya wa "WWE" waja kwa kishindo.Fahamu zaidi hapa.
Ni kizazi kipya kwa upande wa mchezo wa
mieleka kwa sasa kwa kuwa tayari damu changa tunaona zinachukua nafasi
kubwa ya kuwashinda wahusika wakuu ambao wamezoeleka katika tasnia hii
ya mieleka.
Mbabe ambaye… Read More
#MICHEZO>>>BAADA YA XAVI, ETO'O NAYE AMTUPIA DONGO CR7, AMZODOA KUHUSU TUZO ZAKE ZA BALLON D'OR.FAHAMU ZAIDI HAPA.Mshambuliaji
wa zamani wa Barcelona, Samuel Eto'o ambaye kwa sasa ni kocha mchezaji
wa timu ya Antalyaspor ya Uturuki amemzungumzia mchezaji mwenzake wa
zamani wa Xavi Hernandez katika njia ambayo inaonyesha ni dongo kwa s… Read More
#MICHEZO>>>>MAJOGOO WA LIVERPOOL WALIVUNJA DARAJA LA STAMFORD, CHELSEA HOI.FAHAMU ZAIDI HAPA.
Utamu
wa Ligi Kuu ya England ‘Premier League’ umeendelea kuwa mtamu, hiyo ni
baada ya kushuhudia wenyeji wa Daraja la Stamford wakiangukia pua kwa
wageni wao ambao ni maarufu kwa jina la Majogoo.Mabao mawili
yaliy… Read More
0 comments:
Post a Comment