Sunday 27 March 2016

Dogo Janja amchana Young Dee, Amwambia asilete uteja wake kwenye picha za watu.Fahamu zaidi hapa.

Baada ya diss za mtandaoni hatimaye dogo janja amefunguka wazi kuchukizwa na kitendo cha rapa Young dee kudiss post ya Babu tale kuhusu chid benz akimtaka young dee kuacha kuleta #Uteja wake kwenye issue za watu.
Akizungumza na planetbongo dogo janja amesema amechukizwa na kukerwa kitendo cha young dee cha kudiss video ya babu tale iliyoelezea uamuzi wake wa kumsaidia chidi benz ambaye ameathirika na Dawa za kulevya akihoji kwanini young dee alidiss kitendo cha msanii mwenzake kusaidiwa.

Amesema watu wengi walianza kupost picha nyingi za kumdhalilisha chid benz kwa jinsi alivyodhohofika(baada ya kufanya interview ya kwanza na east africa radio)na hakusikia young dee akidiss kuhusu hilo lakini anashangazwa alipodiss video iliyowaonyesha mashabiki na watu wengine kuwa sasa chid benz amepata usaidizi.

Ameongeza kuwa young dee alipaswa kujua mbali na babu tale kuwa meneja lakini pia anaweza kuwa mzazi wake kwahiyo hakupaswa kumdiss kwenye mtandao kama alivyofanya. "Mtu asilete uteja wake kwenye picha za watu"alisema dogo janja.

Teja ni mtu anayetumia dawa za kulevya na dogo janja kwenye post yake instagramme kuhusu young dee lilionekana neno "Young wa kupenga" ambalo kwa maana ya mtaani mtu wa kupenga linamaanisha mtu anayetumia #unga Ambaye mara nyingi hufanya ishara hiyo muda mwingi popote.

Young dee amekuwa akiandamwa na kashfa ya kutumia Dawa za kulevya jambo ambalo mara zote amelikanusha vikali.

Aliwahi kunukuliwa akisema mtu anayetumia unga hajifichi ipo siku itafahamika kwa hiyo watu wasubiri kama ni kweli anatumia itafahamika.
-PlanetBongo

0 comments:

Post a Comment