Sunday 27 March 2016

DOGO JANJA AWAPA ZAWADI YA GARI WAZAZI WAKE.FAHAMU ZAIDI HAPA.

Baada ya Dogo Janja kununuliwa gari mpya aina ya Mercedes Benz na bosi wake Madee na kumfanya kuwa na magari mawili, amedai gari lake la zamani anawapelekea wazazi wake.


Hii ndio gari yake ya zamani ambayo amedai anaipeleka kwa wazazi wake
Akiongea na Bongo5 hivi karibuni, Dogo Janja alisema kwa sasa hawezi kumiliki magari mawili hivyo gari lake la zamani analipeleka kwa wazazi wake.
“Sasa hivi na magari mawili ila ile gari ya zamani itaenda nyumbani kwa wazee ili na wao wakakimbize,” alisema Dogo Janja.
Rapa huyo kwa sasa anafanya vizuri na video yake ya wimbo My Life.

0 comments:

Post a Comment