Wednesday 23 March 2016

TFF YAPIGA MARUFUKU KUCHEZA MCHEZO WA KUBAHATISHA(BETTING).FAHAMU ZAIDI HAPA.

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) inapenda kuwakumbusha wanafamilia wa mpira wa miguu kuto kushiriki katika michezo ya kubahatisha (Betting)juu ya ibara ya 59 kifungu kidogo cha 11 kinachotamka:
TFF Family members shall at all times comply with the following ethical principles "To not take part in betting connected with football and do not tolerate any form of manipulation or unlawful influencing of match results".

Hivyo wanafamilia ya mpira wa miguu Tanzania wanakumbushwa kuheshimu Katiba ya TFF Kwa kutoshiriki katika michezo ya kubahatisha (betting).

Wanafamilia ya TFF ni pamoja na viongozi wa mpira wa ngazi, zote, wachezaji, makocha, waamuzi, makamisaa, waajiriwa wa TFF, wajumbe wa kamati mbali mbali za TFF na wengine wote ambao kwa namna moja au nyingine wanajihusisha na mpira wa miguu

0 comments:

Post a Comment