Tuesday 11 July 2017

Kimenuka....Baada ya Mkuu wa Wilaya ya Hai Kuharibu Shamba Lake, Mbowe amfikisha Mahakamani.

Kampuni ya Kilimanjaro Veggies Ltd inayomilikiwa na Freeman Mbowe, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), imefungua kesi katika Mahakama Kuu, Kanda ya Moshi dhidi ya Mkuu wa Wilaya ya Hai, Gelasius Byakanwa.

Imefungua kesi hiyo dhidi ya mkuu huyo wa wilaya kwa kuwa ndiye anayedaiwa kushiriki uharibifu wa miundombinu ya shamba la mbogamboga inalolimiliki wilayani Hai, Mkoa wa Kilimanjaro.

Kesi hiyo ambayo iko chini ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Kanda ya Moshi, Aishael Sumari, ilifunguliwa Juni 30, mwaka huu na Kampuni ya Uwakili ya D’ Souza& co ya jijini Arusha kwa niaba ya kampuni hiyo.

Kesi hiyo ina mashauri mawili ambayo ni shauri la ardhi namba 20/2017 na maombi madogo namba 51/2017.

Maombi hayo madogo namba 51/2017, yaliletwa kwa hati ya dharura ambapo mdai anaomba zuio la muda liweze kutolewa dhidi ya mdaiwa ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Hai asiweze kufanya chochote katika eneo la shamba la hekari 2.7 lililopo katika Kijiji cha Nshara, Kata ya Machame Kaskazini, wilayani Hai, Mkoa wa Kilimanjaro.

Aidha, katika kesi hiyo, madai ya msingi ni zuio dhidi ya mdaiwa na wafanyakazi au mtu yeyote asiweze kuingilia eneo husika, mdaiwa aombe radhi kwa vitendo alivyovifanya ikiwa ni pamoja na kulipa fidia ya Sh milioni 549.3 kama hasara aliyoipata mlalamikaji.

Mashauri hayo yamepangwa kusikilizwa Julai 13, mwaka huu.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment