Friday 28 July 2017

PENZI ni Kikohozi...Nisha Amuonyesha Mpenzi wake Mpya.

MSANII wa filamu Bongo, Salma Jabu ‘Nisha’ amebadili jina lake na kujiita Nisha Minhal Azad huku kisa kikidaiwa kuwa amefanya hivyo baada ya kuingia katika uhusiano wa kimapenzi na ‘Serengeti Boy’ anayetumia jina hilo.

Kwa mujibu wa chanzo cha karibu na msanii huyo, Nisha amekuwa karibu na ‘Serengeti Boy’ huyo ambaye pia ni msanii wa Bongo Fleva na kwamba ameamua kuanika kabisa uhusiano huo bila kificho.

“Nisha amepata tulizo baada ya kukaa kwa muda mrefu bila kuwa na mwanaume. Huyo mpenzi wake wa sasa ni msanii wa Bongo Fleva anajulikana kwa jina la Minu, yaani Nisha humuelezi chochote juu ya dogo huyo na wanaongozana mara kwa mara,” kilidai chanzo na kuongeza;


“Kwa sasa ameamua kuanika ukweli huo kila kona, kwenye mitandao ya kijamii amebadilisha mpaka jina lake na kujiita Nisha Minhal Azad. Hivi karibuni aliweka picha katika Insta yake akiwa naye katika pozi la mahaba na kuandika; ‘kuna tofauti kubwa kati ya Serengeti na Ngorongoro.’

Baada ya kunasa madai hayo, Ijumaa lilimtafuta Nisha na kumuuliza ukweli juu ya kinachoonekana na kuongelewa, alipopatikana alikiri kubadili jina na kuwa katika uhusiano na Serengeti Boy huyo;
“Ni kweli nipo katika uhusiano na huyo mtu, mengine siwezi kuyaanika ila kifupi ni hivyo.”

Nisha kwa nyakati tofauti aliwahi kuwa katika uhusiano wa kimapenzi na staa wa Bongo Fleva, Emmanuel Elbariki ‘Nay wa Mitego’ pamoja na Baraka Andrew ‘Barakah The Prince’.


Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment