Thursday 27 July 2017

TEGETE AFURAHIA KUTUA MAJIMAJI, ASEMA ANATAKA KUREJESHA MAMBO YAKE.

Jerry Tegete ameonyesha kufurahia kusajiliwa Majimaji ya Songea.

Tegete amesema anaamini Majimaji inakuwa maisha yake mapya ya soka na anatamani kufanya vema.

“Maisha ya soka haujui utaenda wapi, lakini ninataka kurudisha kiwango changu na kufanya vizuri zaidi nikiwa na Majimaji,” alisema.


Tegete ameondoka Mwadui FC na kujiunga na Majimaji ambaye msimu uliopita ilifanya kazi ya ziada kujikomboa isiteremke daraja.

Tegete alikuwa kinara katika ufungaji wakati akiichezea Yanga.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment