Sunday 23 July 2017

Upinzani wapanga migomo na uvunjaji sheria DRC kumuondoa kabila madarakani.

Upinzani wapanga migomo na uvunjaji sheria DRC
Upande wa upinzani katika Jamhuri ya Demokrasi ya Congo, umetangaza mpango wa migomo na kuvunja sheria, kujaribu kumlazimisha Rais Joseph Kabila aondoke madarakani.
Mgomo wa jumla wa siku mbili utaanza tarehe 8 Agosti.
Maandamano ya pamoja yamepangwa kufanywa baadaye mwezi ujao, katika kila jimbo la nchi.
Katika taarifa yake, upinzani umesema, ikiwa Rais Kabila hato-taja siku ya uchaguzi ufikapo mwisho wa mwezi wa Septemba, basi watu waache kulipa kodi kwa serikali.
Muhula wa rais ulima-li-zika mwaka jana.
Makubaliano yaliyofikiwa baada ya Kanisa Katoliki kupatanisha, ni kwamba atabaki madarakani hadi Disemba mwaka huu, lakini rais baadae alisema, hakutoa ahadi yoyote.

Mada zinazohusiana

Chanzo:BBC SWAHILI.
Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment