Friday 11 August 2017

Juma Nature Naye Amgeukia Gigy Money, Amtaka Afunge Mdomo na Asiongee Ongeee.

Msanii Juma Nature amewakingia kifua wasanii wa kike wa zamani ambao Gigy Money amesema walikuwa hakuna cha maana wanachokiimba, na kumtaka atulie kwani bado ni mdogo kwenye tasnia.

Akizungumza na mwandishi wetu Juma Nature amesema kitu ambacho Gigy Money anatakiwa kufanya sasa hivi ni mazoezi ili aweze kuandika nyimbo, na sio kuongea hovyo kuponda watu wazima, kwani hajapitia mikiki kwenye maisha ya muziki.


"Hawezi kuwa na dharau wakati mtu mwenyewe hata albam saba hajafikisha, bado mdogo sana afanye mazoezi atunge nyimbo zenye hekima, anaweza akapata matuzo kibao, lakini asiongee ongee hovyo bado mdogo sana huyo mtoto, hajawahi kupata mikiki, aingie kwenye mikiki mikiki awaulize wenzake kina Zay B  watamfundisha wanawake wenzake, sisi wanaume kwetu ndiyo asiingie kabisa kwa sababu huku vitani", alisema Juma Nature.


Toa Maoni yako Hapa Chini:

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment