Tuesday 22 August 2017

Maneno ya Afande Sele kwa ‘umarioo’ Asema Unapunguza Nguvu za Kiume.

Msanii mkongwe wa Bongo Flava, Afande Sele amedai kuwa vijana wa kiume kujihusisha katika mapenzi na wakubwa zao ili kusaidiwa kiuchumi ni moja wa sabubu zinazopelekea upungufu wa nguvu za kiume.

Afande Sele ameeleza kuwa kitendo hicho kinamnyima uhuru binafsi muhusika kwa sababu unapokaa na mtu ambaye kila kitu unamtengemea unakosa uhuru wa maisha.

“Hata uwezo wako wa kufikiri unapungua kwa sababu unajikuta muda mwingi unafikiria kumfurahisha mtu. Muda mwingine hata mapenzi unakuta hujisikii kwa sababu mapenzi nayo ni ratiba lakini kwa sababu unaishi na mtu anakulea utafanya tu,” ameiambia Planet Bongo ya EA Radio na kuongeza.

“Ndio maana leo hii suala la nguvu za kiume limekuwa ni agenda kubwa kwa sababu wanafanya vitu na watu siyo machaguo yao ila wakijiari kwenye vitu kama kilimo watakuwa na maisha ya uhuru sana,” amesisitiza.

Download  Application ya Hebron Malele Blog Kwenye Simu yako Kusoma Habari Zetu Kwa Urahisi>>>>Bonyeza Hapa

                            Follow me instagram>>>Bonyeza Hapa
                       Facebook page like hapa>>>Bonyeza Hapa
                       Jiunge na group la whatsapp>>>Bonyeza Hapa

0 comments:

Post a Comment